-
Mathayo 22:42-45Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
42 “Mna maoni gani kuhusu Kristo? Ni mwana wa nani?” Wakamwambia: “Wa Daudi.”+ 43 Akawauliza: “Basi, kwa nini Daudi akiongozwa na roho+ anamwita Bwana, akisema, 44 ‘Yehova* alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke maadui wako chini ya miguu yako”’?+ 45 Basi ikiwa Daudi anamwita Bwana, anawezaje kuwa mwanawe?”+
-
-
Luka 20:41-44Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
41 Naye akawauliza: “Kwa nini watu husema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?+ 42 Kwa maana Daudi mwenyewe anasema katika kitabu cha Zaburi, ‘Yehova* alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume 43 mpaka niwaweke maadui wako kuwa kiti cha miguu yako.”’+ 44 Basi, Daudi anamwita Bwana; kwa hiyo anawezaje kuwa mwanawe?”
-