Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 22:41-46
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 41 Basi Mafarisayo walipokuwa wamekusanyika, Yesu akawauliza:+ 42 “Mna maoni gani kuhusu Kristo? Ni mwana wa nani?” Wakamwambia: “Wa Daudi.”+ 43 Akawauliza: “Basi, kwa nini Daudi akiongozwa na roho+ anamwita Bwana, akisema, 44 ‘Yehova* alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke maadui wako chini ya miguu yako”’?+ 45 Basi ikiwa Daudi anamwita Bwana, anawezaje kuwa mwanawe?”+ 46 Na hakuna mtu aliyeweza kumjibu neno, na tangu siku hiyo hakuna mtu aliyethubutu tena kumuuliza swali.

  • Marko 12:35-37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Hata hivyo, Yesu akiendelea kufundisha hekaluni, akawauliza: “Kwa nini waandishi husema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?+ 36 Kupitia roho takatifu+ Daudi mwenyewe alisema, ‘Yehova* alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke maadui wako chini ya miguu yako.”’+ 37 Daudi mwenyewe anamwita Bwana, basi Kristo anawezaje kuwa mwanawe?”+

      Na umati mkubwa ulikuwa ukimsikiliza kwa furaha.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki