-
Mathayo 22:41-46Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
41 Basi Mafarisayo walipokuwa wamekusanyika, Yesu akawauliza:+ 42 “Mna maoni gani kuhusu Kristo? Ni mwana wa nani?” Wakamwambia: “Wa Daudi.”+ 43 Akawauliza: “Basi, kwa nini Daudi akiongozwa na roho+ anamwita Bwana, akisema, 44 ‘Yehova* alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke maadui wako chini ya miguu yako”’?+ 45 Basi ikiwa Daudi anamwita Bwana, anawezaje kuwa mwanawe?”+ 46 Na hakuna mtu aliyeweza kumjibu neno, na tangu siku hiyo hakuna mtu aliyethubutu tena kumuuliza swali.
-
-
Marko 12:35-37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
35 Hata hivyo, Yesu akiendelea kufundisha hekaluni, akawauliza: “Kwa nini waandishi husema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?+ 36 Kupitia roho takatifu+ Daudi mwenyewe alisema, ‘Yehova* alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke maadui wako chini ya miguu yako.”’+ 37 Daudi mwenyewe anamwita Bwana, basi Kristo anawezaje kuwa mwanawe?”+
Na umati mkubwa ulikuwa ukimsikiliza kwa furaha.
-