-
Marko 12:35-37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
35 Hata hivyo, Yesu akiendelea kufundisha hekaluni, akawauliza: “Kwa nini waandishi husema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?+ 36 Kupitia roho takatifu+ Daudi mwenyewe alisema, ‘Yehova* alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke maadui wako chini ya miguu yako.”’+ 37 Daudi mwenyewe anamwita Bwana, basi Kristo anawezaje kuwa mwanawe?”+
Na umati mkubwa ulikuwa ukimsikiliza kwa furaha.
-
-
Luka 20:41-44Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
41 Naye akawauliza: “Kwa nini watu husema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?+ 42 Kwa maana Daudi mwenyewe anasema katika kitabu cha Zaburi, ‘Yehova* alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume 43 mpaka niwaweke maadui wako kuwa kiti cha miguu yako.”’+ 44 Basi, Daudi anamwita Bwana; kwa hiyo anawezaje kuwa mwanawe?”
-