-
Mathayo 13:3-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Ndipo akawaambia mambo mengi kwa kutumia mifano,+ akisema: “Tazama! Mpandaji alienda kupanda mbegu.+ 4 Alipokuwa akipanda, mbegu fulani zikaanguka kando ya barabara, ndege wakaja na kuzila.+ 5 Nyingine zikaanguka kwenye miamba, mahali pasipo na udongo mwingi, na mara moja zikachipuka kwa sababu udongo haukuwa na kina.+ 6 Lakini jua lilipochomoza, ziliungua na kunyauka kwa sababu hazikuwa na mizizi. 7 Nyingine zikaanguka kwenye miiba, nayo miiba ikakua na kuzisonga.+ 8 Mbegu nyingine zikaanguka kwenye udongo mzuri nazo zikaanza kuzaa matunda, nyingine mara 100 zaidi, nyingine 60, na nyingine 30.+ 9 Aliye na masikio na asikilize.”+
-
-
Luka 8:5-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 “Mpandaji alienda kupanda mbegu. Alipokuwa akipanda, mbegu fulani zikaanguka kando ya barabara zikakanyagwa-kanyagwa, na ndege wa angani wakazila.+ 6 Nyingine zikaanguka kwenye mwamba, na baada ya kuchipuka, zikakauka kwa kukosa maji.+ 7 Nyingine zikaanguka kwenye miiba, nayo miiba ikakua pamoja nazo na kuzisonga.+ 8 Lakini nyingine zikaanguka kwenye udongo mzuri, zikachipuka na kuzaa matunda mara 100 zaidi.”+ Baada ya kusema hayo, akasema kwa sauti kubwa: “Yule aliye na masikio ya kusikiliza, na asikilize.”+
-