5Sasa Naamani, mkuu wa jeshi la mfalme wa Siria, alikuwa mtu maarufu aliyeheshimiwa na bwana wake, kwa sababu Yehova alikuwa amewapa Wasiria ushindi* kupitia yeye. Alikuwa shujaa hodari, ingawa alikuwa na ukoma.*
14 Ndipo akashuka mtoni na kujitumbukiza* mara saba katika Mto Yordani, kama alivyosema mtu wa Mungu wa kweli.+ Kisha mwili wake ukaponywa ukawa kama mwili wa mvulana mdogo,+ akawa safi.+