-
Yohana 5:6-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Yesu alipomwona mtu huyo amelala hapo, na akijua kwamba alikuwa mgonjwa kwa muda mrefu, akamuuliza: “Je, unataka kupona?”+ 7 Mgonjwa huyo akamjibu: “Bwana, sina mtu wa kuniweka ndani ya dimbwi maji yanapotibuliwa, lakini ninapotaka kuingia, mtu mwingine huingia kabla yangu.” 8 Yesu akamwambia: “Simama! Chukua mkeka wako,* utembee.”+ 9 Mtu huyo akapona mara moja, akabeba mkeka wake* na kuanza kutembea.
Hiyo ilikuwa siku ya Sabato.
-