-
Mathayo 11:7-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Hao walipoondoka, Yesu akaanza kuuambia umati kumhusu Yohana: “Mlienda nyikani kuona nini?+ Tete likitikiswa na upepo?+ 8 Basi, mlienda kuona nini? Mtu aliyevaa mavazi laini?* Kwa maana wale wanaovaa mavazi laini wamo katika nyumba za wafalme. 9 Basi kwa kweli, kwa nini mlienda? Kumwona nabii? Ndiyo, ninawaambia, mtu aliye zaidi ya nabii.+ 10 Huyu ndiye ambaye imeandikwa hivi kumhusu: ‘Tazama! Ninamtuma mjumbe wangu mbele yako,* ili akutayarishie njia mbele yako!’+ 11 Kwa kweli ninawaambia, kati ya wale waliozaliwa na wanawake hajatokea mtu mkuu kuliko Yohana Mbatizaji, lakini mtu mdogo zaidi katika Ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.+
-