-
Mathayo 13:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Siku hiyo Yesu akatoka ndani ya nyumba na kuketi kando ya bahari. 2 Na umati mkubwa sana ukakusanyika karibu naye hivi kwamba akapanda ndani ya mashua na kuketi, na umati wote ulikuwa umesimama ufuoni.+ 3 Ndipo akawaambia mambo mengi kwa kutumia mifano,+ akisema: “Tazama! Mpandaji alienda kupanda mbegu.+
-
-
Marko 4:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Yesu akaanza tena kufundisha kando ya bahari, na umati mkubwa sana ukakusanyika karibu naye. Basi akapanda ndani ya mashua na kuketi humo mbali kidogo na ufuo, lakini umati wote ulikuwa kando ya bahari, ufuoni.+ 2 Naye akaanza kuwafundisha mambo mengi kwa mifano,+ na alipokuwa akifundisha akasema:+
-