-
Marko 5:18-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Alipokuwa akipanda mashua, yule mtu aliyekuwa na roho waovu akaanza kumsihi aende pamoja naye.+ 19 Hata hivyo, hakumruhusu, bali alimwambia: “Nenda nyumbani kwa watu wako wa ukoo, ukawaambie mambo yote ambayo Yehova* amekufanyia na jinsi alivyokuonyesha rehema.” 20 Mtu huyo akaenda zake akaanza kutangaza katika Dekapoli* mambo yote ambayo Yesu alimfanyia, na watu wote wakashangaa.
-