-
Mathayo 9:20-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Na tazama! mwanamke aliyekuwa na mtiririko wa damu+ kwa miaka 12 akaja kutoka nyuma na kugusa upindo wa vazi lake la nje,+ 21 kwa maana alikuwa akijiambia: “Nikigusa tu vazi lake la nje, nitapona.” 22 Yesu akageuka, na alipomwona, akamwambia: “Binti, usiogope! Imani yako imekuponya.”+ Na kutoka saa hiyo, yule mwanamke akapona.+
-
-
Marko 5:25-29Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Sasa kuna mwanamke aliyekuwa na mtiririko wa damu+ kwa miaka 12.+ 26 Alikuwa ameteseka sana* mikononi mwa madaktari wengi na alikuwa ametumia mali yake yote, na hakuwa amepona, badala yake hali yake ilizidi kuwa mbaya. 27 Aliposikia kumhusu Yesu, akapenya katika umati nyuma ya Yesu na kuligusa vazi lake la nje,+ 28 kwa maana alikuwa akisema: “Nikiyagusa tu mavazi yake ya nje, nitapona.”+ 29 Papo hapo mtiririko wake wa damu ukakoma, naye akahisi mwilini mwake kwamba alikuwa amepona ule ugonjwa mbaya.
-