-
Marko 5:25-34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Sasa kuna mwanamke aliyekuwa na mtiririko wa damu+ kwa miaka 12.+ 26 Alikuwa ameteseka sana* mikononi mwa madaktari wengi na alikuwa ametumia mali yake yote, na hakuwa amepona, badala yake hali yake ilizidi kuwa mbaya. 27 Aliposikia kumhusu Yesu, akapenya katika umati nyuma ya Yesu na kuligusa vazi lake la nje,+ 28 kwa maana alikuwa akisema: “Nikiyagusa tu mavazi yake ya nje, nitapona.”+ 29 Papo hapo mtiririko wake wa damu ukakoma, naye akahisi mwilini mwake kwamba alikuwa amepona ule ugonjwa mbaya.
30 Mara moja Yesu akahisi ndani yake kwamba nguvu+ zimemtoka, akaugeukia umati na kuuliza: “Ni nani aliyegusa mavazi yangu ya nje?”+ 31 Lakini wanafunzi wake wakamwambia: “Unaona jinsi umati unavyokusonga, na unauliza, ‘Ni nani aliyenigusa?’” 32 Hata hivyo, alikuwa akitazama ili aone mtu aliyekuwa amefanya hivyo. 33 Yule mwanamke akijua lililompata, akaja akitetemeka kwa hofu akaanguka chini mbele yake, akamwambia ukweli wote. 34 Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani,+ umepona ugonjwa wako mbaya.”+
-
-
Luka 8:43-48Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
43 Kulikuwa na mwanamke aliyekuwa na mtiririko wa damu+ kwa miaka 12, na hakuwa amepata mtu wa kumponya.+ 44 Akaja kutoka nyuma na kugusa upindo wa vazi lake la nje,+ na mara moja akaacha kutokwa damu. 45 Ndipo Yesu akauliza: “Ni nani aliyenigusa?” Wote walipokuwa wakikana, Petro akasema: “Mwalimu, umati umekuzunguka na kukusonga.”+ 46 Lakini Yesu akasema: “Mtu fulani amenigusa, kwa maana ninajua nguvu+ zimenitoka.” 47 Yule mwanamke alipoona kwamba hakuepuka kutambuliwa, akaja akitetemeka na kuanguka chini mbele yake, akaeleza mbele ya watu wote sababu iliyomfanya amguse na jinsi alivyoponywa mara moja. 48 Lakini Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”+
-