-
Marko 5:30-34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Mara moja Yesu akahisi ndani yake kwamba nguvu+ zimemtoka, akaugeukia umati na kuuliza: “Ni nani aliyegusa mavazi yangu ya nje?”+ 31 Lakini wanafunzi wake wakamwambia: “Unaona jinsi umati unavyokusonga, na unauliza, ‘Ni nani aliyenigusa?’” 32 Hata hivyo, alikuwa akitazama ili aone mtu aliyekuwa amefanya hivyo. 33 Yule mwanamke akijua lililompata, akaja akitetemeka kwa hofu akaanguka chini mbele yake, akamwambia ukweli wote. 34 Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani,+ umepona ugonjwa wako mbaya.”+
-