-
Luka 8:45-48Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
45 Ndipo Yesu akauliza: “Ni nani aliyenigusa?” Wote walipokuwa wakikana, Petro akasema: “Mwalimu, umati umekuzunguka na kukusonga.”+ 46 Lakini Yesu akasema: “Mtu fulani amenigusa, kwa maana ninajua nguvu+ zimenitoka.” 47 Yule mwanamke alipoona kwamba hakuepuka kutambuliwa, akaja akitetemeka na kuanguka chini mbele yake, akaeleza mbele ya watu wote sababu iliyomfanya amguse na jinsi alivyoponywa mara moja. 48 Lakini Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”+
-