Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 9:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Na tazama! mwanamke aliyekuwa na mtiririko wa damu+ kwa miaka 12 akaja kutoka nyuma na kugusa upindo wa vazi lake la nje,+

  • Marko 5:25-28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Sasa kuna mwanamke aliyekuwa na mtiririko wa damu+ kwa miaka 12.+⁠ 26 Alikuwa ameteseka sana* mikononi mwa madaktari wengi na alikuwa ametumia mali yake yote, na hakuwa amepona, badala yake hali yake ilizidi kuwa mbaya. 27 Aliposikia kumhusu Yesu, akapenya katika umati nyuma ya Yesu na kuligusa vazi lake la nje,+ 28 kwa maana alikuwa akisema: “Nikiyagusa tu mavazi yake ya nje, nitapona.”+

  • Luka 8:43, 44
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 43 Kulikuwa na mwanamke aliyekuwa na mtiririko wa damu+ kwa miaka 12, na hakuwa amepata mtu wa kumponya.+ 44 Akaja kutoka nyuma na kugusa upindo wa vazi lake la nje,+ na mara moja akaacha kutokwa damu.

  • Matendo 19:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Na Mungu akaendelea kufanya matendo yenye nguvu yasiyo ya kawaida kupitia mikono ya Paulo,+ 12 hivi kwamba hata nguo na vitambaa vilivyogusa mwili wake vilipelekewa wagonjwa,+ nao wakaponywa magonjwa, na roho waovu wakatoka.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki