-
Marko 6:14-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Mfalme Herode akasikia habari hizo, kwa maana jina la Yesu lilijulikana sana na watu walikuwa wakisema: “Yohana Mbatizaji amefufuliwa kutoka kwa wafu, ndiyo sababu anafanya matendo yenye nguvu.”+ 15 Lakini wengine walikuwa wakisema: “Ni Eliya.” Pia, wengine wakasema: “Ni nabii kama manabii wa kale.”+ 16 Lakini Herode alipopata habari hizo akasema: “Yule Yohana niliyemkata kichwa, amefufuliwa.”
-