-
Yakobo 4:13-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Haya, basi, ninyi mnaosema: “Leo au kesho tutasafiri kwenda jiji fulani nasi tutakaa mwaka mmoja huko, tutafanya biashara na kupata faida,”+ 14 ingawa hamjui jinsi maisha yenu yatakavyokuwa kesho.+ Kwa maana ninyi ni ukungu unaotokea kwa muda kidogo na kisha kutoweka.+ 15 Badala yake, mnapaswa kusema: “Yehova* akipenda,+ tutaishi na kufanya hili au lile.” 16 Lakini sasa mnajivuna na kujigamba kwa kiburi. Majivuno yote ya namna hiyo ni maovu.
-