-
Zaburi 49:16-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Usiogope mtu anapotajirika,
Fahari ya nyumba yake ikiongezeka,
17 Kwa maana akifa hawezi kwenda na kitu chochote;+
Fahari yake haitashuka shimoni pamoja naye.+
18 Kwa maana wakati wa maisha yake anajipongeza mwenyewe.+
(Watu hukusifu unapopata ufanisi.)+
19 Lakini mwishowe hujiunga na kizazi cha mababu zake.
Hawataona nuru tena kamwe.
-