26 Kisha Mungu akasema: “Na tufanye+ mtu kwa mfano+ wetu, kulingana na sura+ yetu, nao watawale samaki wa baharini na viumbe wanaoruka angani na wanyama wa kufugwa na dunia yote na kila mnyama anayetambaa duniani.”+
6 kwa kweli kwetu kuna Mungu mmoja+ aliye Baba,+ ambaye vitu vyote vimetoka kwake na sisi kwa ajili yake;+ na kuna Bwana mmoja, Yesu Kristo, ambaye vitu vyote vimepitia kwake+ na sisi kupitia kwake.
16 kwa sababu kupitia kwake vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani, vitu vinavyoonekana na vitu visivyoonekana,+ iwe ni viti vya ufalme au utawala au serikali au mamlaka. Vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia kwake+ na kwa ajili yake.
2 Lakini sasa mwishoni mwa siku hizi amezungumza nasi kupitia Mwana,+ aliyemweka rasmi kuwa mrithi wa vitu vyote,+ na kupitia kwake aliifanya mifumo ya mambo.*+