Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 26:6-10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Yesu alipokuwa Bethania katika nyumba ya Simoni mwenye ukoma,+ 7 mwanamke fulani aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye mafuta ghali yenye marashi akamkaribia, akaanza kuyamimina juu ya kichwa cha Yesu alipokuwa akila.* 8 Walipoona hilo wanafunzi wakakasirika na kusema: “Hasara hii ni ya nini? 9 Kwa maana mafuta haya yangeuzwa kwa kiasi kikubwa cha pesa na kupewa maskini.” 10 Akijua jambo hilo, Yesu akawaambia: “Kwa nini mnataka kumsumbua mwanamke huyu? Amenitendea jambo jema.

  • Marko 14:3-6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Alipokuwa Bethania akila* katika nyumba ya Simoni mwenye ukoma, mwanamke fulani akaja na chupa ya alabasta iliyokuwa na mafuta yenye marashi, nardo halisi, ghali sana. Akaifungua na kuanza kuyamimina juu ya kichwa cha Yesu.+ 4 Ndipo baadhi yao wakakasirika na kuambiana: “Kwa nini mafuta haya ya marashi yapotezwe bure? 5 Kwa maana mafuta haya yangeuzwa kwa zaidi ya dinari* 300 na maskini wapewe pesa hizo!” Nao wakamkasirikia* sana mwanamke huyo. 6 Lakini Yesu akawaambia: “Mwacheni. Kwa nini mnataka kumsumbua? Amenitendea jambo jema.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki