-
Mathayo 26:6-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Yesu alipokuwa Bethania katika nyumba ya Simoni mwenye ukoma,+ 7 mwanamke fulani aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye mafuta ghali yenye marashi akamkaribia, akaanza kuyamimina juu ya kichwa cha Yesu alipokuwa akila.* 8 Walipoona hilo wanafunzi wakakasirika na kusema: “Hasara hii ni ya nini? 9 Kwa maana mafuta haya yangeuzwa kwa kiasi kikubwa cha pesa na kupewa maskini.”
-
-
Yohana 12:2-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Basi, wakamwandalia mlo wa jioni huko, na Martha alikuwa akiwahudumia,+ lakini Lazaro alikuwa miongoni mwa wale waliokuwa wakila* pamoja na Yesu. 3 Kisha Maria akachukua ratili* moja ya mafuta yenye marashi, nardo halisi, ghali sana, akammiminia Yesu miguuni na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba ikajaa harufu ya mafuta yenye marashi.+ 4 Lakini Yuda Iskariote,+ mmoja wa wanafunzi wake aliyekuwa karibu kumsaliti akasema: 5 “Kwa nini mafuta haya yenye marashi hayangeuzwa kwa dinari* 300 na maskini wapewe pesa hizo?”
-