11 Na bado baadhi yenu mlikuwa hivyo. Lakini mmeoshwa mkawa safi;+ mmetakaswa;+ mmetangazwa kuwa waadilifu+ katika jina la Bwana Yesu Kristo na kwa roho ya Mungu wetu.
25 Enyi waume, endeleeni kuwapenda wake zenu,+ kama vile Kristo pia alivyolipenda kutaniko na kujitoa mwenyewe kwa ajili yake,+26 ili alitakase, akilisafisha na kuliosha kwa maji kupitia neno,+
5 (si kwa sababu ya matendo yoyote ya uadilifu tuliyokuwa tumefanya,+ bali kwa sababu ya rehema yake),+ alituokoa kupitia kuoshwa kulikotuleta kwenye uzima,+ na kwa kutufanya wapya kupitia roho takatifu.+
22 acheni tukaribie tukiwa na mioyo minyoofu na imani kamili, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa na kuwa safi kutokana na dhamiri yenye uovu+ na miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.+