19 Hata hivyo, mtakapopelekwa, msihangaike kuhusu jambo mtakalosema au jinsi mtakavyolisema, kwa sababu mtapewa jambo la kusema katika saa hiyo;+20 kwa maana si ninyi tu mnaosema, bali ni roho ya Baba yenu inayosema kupitia ninyi.+
13 Hata hivyo, huyo* atakapokuja, roho ya ile kweli,+ atawaongoza ninyi kwenye kweli yote, kwa maana hatasema kwa uamuzi wake mwenyewe, bali atasema mambo anayosikia, naye atawatangazia mambo yanayokuja.+
27 Kutiwa mafuta ambako mlipokea kutoka kwake+ hukaa ndani yenu, na hamhitaji kufundishwa na yeyote; lakini kutiwa mafuta kutoka kwake kunawafundisha kuhusu mambo yote,+ na ni kweli si uwongo. Kama kulivyowafundisha ninyi, kaeni katika muungano na yeye.+