21 Yehova akamkumbuka Sara kama alivyokuwa amesema, na Yehova akamtendea Sara jambo alilokuwa amemwahidi.+ 2 Basi Sara akapata mimba+ Abrahamu akiwa mzee, akamzalia mwana wakati uleule ambao Mungu alikuwa amemwahidi Abrahamu.+ 3 Abrahamu akamwita Isaka, mwana huyo ambaye Sara alikuwa amemzalia.+