Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matendo 20:22, 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Na sasa, tazameni! nikiwa nimefungwa katika* roho, ninasafiri kwenda Yerusalemu, ingawa sijui mambo yatakayonipata huko, 23 isipokuwa kutoka jiji mpaka jiji roho takatifu inanitolea ushahidi tena na tena, ikisema kwamba nitafungwa gerezani na kupatwa na dhiki.+

  • Matendo 21:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Akaja mahali tulipokuwa akachukua mshipi wa Paulo, akajifunga miguu na mikono na kusema: “Hivi ndivyo roho takatifu inavyosema, ‘Wayahudi kule Yerusalemu watamfunga+ hivi mwanamume ambaye mshipi huu ni wake, nao watamtia mikononi mwa watu wa mataifa.’”+

  • 2 Wakorintho 11:23-28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Je, wao ni wahudumu wa Kristo? Ninajibu kama mwendawazimu, mimi ni mhudumu kwa njia kubwa hata zaidi: Nimefanya kazi nyingi zaidi,+ nimefungwa gerezani mara nyingi zaidi,+ nimepigwa mara nyingi sana, na kukaribia kufa mara nyingi.+ 24 Mara tano nilipigwa na Wayahudi viboko 40 kasoro kimoja,+ 25 mara tatu nilipigwa kwa fimbo,+ mara moja nilipigwa mawe,+ mara tatu nilivunjikiwa na meli,+ usiku mmoja na mchana mmoja nimekaa baharini; 26 mara nyingi katika safari, hatari za kutokana na mito, hatari za kutokana na wezi, hatari za kutokana na watu wangu mwenyewe,+ hatari za kutokana na mataifa,+ hatari jijini,+ hatari nyikani, hatari baharini, hatari kati ya ndugu wa uwongo, 27 kwa kazi ngumu na yenye kutaabisha, mara nyingi kukosa usingizi usiku,+ njaa na kiu,+ kukosa chakula mara nyingi,+ na pia baridi na kukosa mavazi.*

      28 Zaidi ya mambo hayo ya nje, pia kuna jambo linalonipata siku kwa siku:* kuhangaikia makutaniko yote.+

  • Wakolosai 1:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Ninashangilia sasa katika mateso yangu kwa ajili yenu,+ nami ninakabili dhiki za Kristo ambazo bado hazimo katika mwili wangu kwa ajili ya mwili wake,+ ambao ni kutaniko.+

  • 2 Timotheo 1:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Ndiyo sababu ninavumilia pia mambo haya,+ lakini sioni aibu.+ Kwa maana ninamjua Yule ambaye nimemwamini, nami nina uhakika kwamba anaweza kulinda kile nilichoweka amana kwake mpaka siku hiyo.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki