-
Yohana 19:40-42Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
40 Basi wakauchukua mwili wa Yesu na kuufunga kwa vitambaa vya kitani pamoja na manukato,+ kulingana na desturi ya mazishi ya Wayahudi. 41 Ilitukia kwamba kulikuwa na bustani mahali alipouawa,* na katika bustani hiyo kulikuwa na kaburi*+ jipya ambamo hakuna mtu alikuwa amewahi kulazwa. 42 Kwa sababu ilikuwa siku ya Matayarisho+ ya Wayahudi na kaburi lilikuwa hapo karibu, wakamlaza Yesu humo.
-