-
Matendo 16:19-21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Basi, mabwana zake walipoona kwamba wamepoteza tumaini lao la kupata faida,+ wakawakamata Paulo na Sila wakawakokota hadi sokoni kwa watawala.+ 20 Wakawapeleka kwa mahakimu wa raia, na kusema: “Watu hawa wanasumbua sana jiji letu.+ Wao ni Wayahudi, 21 nao wanatangaza desturi ambazo si halali kwetu kuzikubali au kuzifuata, kwa kuwa sisi ni Waroma.”
-