3 Ndipo Sauli akaanza kulishambulia kutaniko. Alikuwa akivamia nyumba moja baada ya nyingine, akiwakokota nje wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani.+
13 Bila shaka, mlisikia kuhusu mwenendo wangu wa zamani katika dini ya Kiyahudi,+ kwamba niliendelea kulitesa sana* kutaniko la Mungu na kuliangamiza;+
13 ingawa zamani nilikuwa mkufuru na mtesaji na mtu mwenye dharau.+ Hata hivyo, nilionyeshwa rehema, kwa sababu nilitenda bila ujuzi na sikuwa na imani.