-
2 Wakorintho 8:1-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Basi akina ndugu, tunawajulisha kuhusu fadhili zisizostahiliwa za Mungu ambazo makutaniko ya Makedonia+ yamepewa. 2 Wakati wa majaribu makali chini ya mateso, shangwe yao nyingi na umaskini mkubwa ulifanya utajiri wa ukarimu wao uwe mwingi.* 3 Kwa maana ilikuwa kulingana na uwezo wao,+ ndiyo, ninashuhudia, hata kupita uwezo wao,+ 4 nao kwa kupenda kwao wenyewe waliendelea kutuomba sana wapate pendeleo la kutoa kwa fadhili, ili washiriki katika huduma ya kutoa msaada kwa ajili ya watakatifu.+
-
-
2 Wakorintho 9:2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 kwa maana ninajua utayari wenu ambao ninajisifia kwa Wamakedonia, kwamba Akaya imekuwa tayari kwa mwaka mmoja sasa, na bidii yenu imewachochea wengi kati yao.
-