-
Waroma 16:25, 26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Sasa kwa Yule anayeweza kuwaimarisha ninyi kulingana na habari njema ninayotangaza na kuhubiriwa kwa Yesu Kristo, kulingana na ufunuo wa siri takatifu+ ambayo ilikuwa imefichwa tangu nyakati za zamani 26 lakini sasa imeonyeshwa wazi* na kujulishwa kupitia Maandiko ya kinabii kati ya mataifa yote kulingana na amri ya Mungu anayedumu milele, ili kuendeleza utii kwa imani;
-
-
Waefeso 3:8, 9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Mimi, niliye mdogo kuliko aliye mdogo zaidi kati ya watakatifu wote,+ nilipewa fadhili hizi zisizostahiliwa,+ ili niwatangazie mataifa habari njema kuhusu utajiri usiopimika wa Kristo 9 na kufanya kila mtu aone usimamizi wa siri takatifu+ ambayo imefichwa kwa vizazi na vizazi katika Mungu, aliyeumba vitu vyote.
-