-
Kutoka 34:33-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Musa alipomaliza kuongea nao, alikuwa akiufunika uso wake kwa kitambaa.+ 34 Lakini kila mara Musa alipoingia ndani mbele za Yehova ili kuongea naye, alikivua kitambaa hicho lakini alijifunika alipotoka nje.+ Alipotoka nje aliwajulisha Waisraeli amri zote alizopewa.+ 35 Nao Waisraeli waliona kwamba ngozi ya uso wa Musa ilitoa miale; basi Musa alijifunika tena kitambaa hicho usoni alipotoka na kukivua alipoingia kuzungumza na Mungu.+
-