-
Waefeso 3:5-7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Katika vizazi vingine wanadamu hawakujulishwa siri hii kama vile ambavyo sasa imefunuliwa kwa mitume wake watakatifu na manabii kupitia roho,+ 6 yaani, kwamba watu wa mataifa, katika muungano na Kristo Yesu na kupitia habari njema, wawe warithi na viungo vya mwili uleule+ na washiriki wa ahadi pamoja nasi. 7 Mimi nilikuja kuwa mhudumu wa hilo kulingana na zawadi ya bure ya Mungu ya fadhili zisizostahiliwa nilizopewa kupitia utendaji wa nguvu zake.+
-