29 Ninajua kwamba nitakapoondoka mbwamwitu wenye kukandamiza wataingia miongoni mwenu+ nao hawatalitendea kundi kwa wororo, 30 na kutoka miongoni mwenu watu watasimama na kusema mambo yaliyopotoka ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.+
18 Kwanza kabisa, nasikia kwamba mnapokutana katika kutaniko, kuna migawanyiko kati yenu; na kwa kadiri fulani ninaamini jambo hilo. 19 Kwa maana lazima kutakuwa na madhehebu miongoni mwenu,+ ili wale waliokubaliwa kati yenu waonekane.
18 Watoto wadogo, ni saa ya mwisho, na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga-Kristo anakuja,+ hata sasa wapinga-Kristo wengi wametokea,+ na kwa sababu hiyo tunajua kwamba ni saa ya mwisho.