-
Mwanzo 27:38-40Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
38 Esau akamwambia baba yake: “Baba, je, una baraka moja tu? Nibariki mimi, naam, mimi pia, baba yangu!” Ndipo Esau akalia kwa sauti kubwa na kububujikwa na machozi.+ 39 Basi Isaka baba yake akamwambia:
“Tazama, makao yako yatakuwa mbali na udongo wenye rutuba duniani, na mbali na umande wa mbingu.+ 40 Na kwa upanga wako utaishi,+ nawe utamtumikia ndugu yako.+ Lakini utakaposhindwa kuvumilia, hakika utaivunja nira yake kutoka shingoni mwako.”+
-