-
Hesabu 14:28-30Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
28 Waambie, ‘“Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Yehova, “nitawatendea mambo yaleyale niliyosikia mkisema!+ 29 Maiti zenu zitaanguka katika nyika hii,+ naam, ninyi nyote mlioninung’unikia, kila mtu aliyeandikishwa mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi.+ 30 Hakuna hata mmoja wenu atakayeingia katika nchi niliyoapa kwamba mtaishi ndani yake,+ isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+
-