Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 26:63, 64
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 63 Hao ndio walioandikishwa na Musa na kuhani Eleazari walipowaandikisha Waisraeli katika jangwa tambarare la Moabu karibu na Yordani huko Yeriko. 64 Lakini hakuna hata mmoja wao aliyeandikishwa na Musa na kuhani Haruni wakati walipowahesabu Waisraeli katika nyika ya Sinai.+

  • Hesabu 32:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 ‘Wanaume waliotoka Misri wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi hawataiona nchi+ ambayo niliapa kwamba nitampa Abrahamu, Isaka, na Yakobo,+ kwa sababu hawakunifuata kwa moyo wote—

  • Kumbukumbu la Torati 1:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 ‘Hakuna mtu hata mmoja wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kwamba nitawapa baba zenu,+

  • Zaburi 95:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu:

      “Hawataingia katika pumziko langu.”+

  • Zaburi 106:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Kwa hiyo akainua mkono wake na kuapa kuwahusu

      Kwamba angewaangusha nyikani;+

  • Waebrania 3:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Naye aliapa kwa akina nani kwamba hawataingia katika pumziko lake? Je, si wale waliotenda kwa kutotii?

  • Waebrania 4:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kwa maana sisi ambao tumeonyesha imani tunaingia katika pumziko, kama alivyosema: “Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu, ‘Hawataingia katika pumziko langu,’”+ ingawa kazi zake zilimalizika tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki