-
Waebrania 10:19-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Kwa hiyo, akina ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri* wa njia ya kuingia katika mahali patakatifu+ kwa damu ya Yesu, 20 aliyotufungulia* kuwa njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia,+ yaani, mwili wake, 21 na kwa kuwa tuna kuhani mkuu aliye juu ya nyumba ya Mungu,+ 22 acheni tukaribie tukiwa na mioyo minyoofu na imani kamili, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa na kuwa safi kutokana na dhamiri yenye uovu+ na miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.+
-