Wimbo wa Safari za Kupanda.
123 Nayainua macho yangu kukuelekea wewe,+
Wewe unayeketi kwenye kiti cha ufalme mbinguni.
2 Kama macho ya watumishi yanavyoutazama mkono wa bwana wao,
Na macho ya kijakazi yanavyoutazama mkono wa bimkubwa wake,
Ndivyo macho yetu yanavyokutazama wewe, Ee Yehova Mungu wetu+
Mpaka utakapotuonyesha kibali.+
3 Tuonyeshe kibali, Ee Yehova, tuonyeshe kibali,
Kwa maana tumedharauliwa vya kutosha.+
4 Tumedhihakiwa vya kutosha na watu wanaojitumaini
Na kudharauliwa na wenye kiburi.