Upendo Unawasukuma Kufanya Hivyo
● Katika Mali, Afrika Magharibi, kunao mashahidi wa Yehova wachache. Wengi wao wanatembea maili sita kwa miguu ili kuhudhuria mikutano. Wakijali sana hali ya kiroho ya watu, Wazungu wawili na Mwafrika mmoja walijitolea kutumikia huko. Kila mmoja anajitoa kufanya saa 200 kila mwezi katika kutangaza kweli za Biblia. Ingawa joto ni jingi sana, wanaona kazi yao ya upendo kuwa yenye maana kustahili wafanye hivyo. Wafanya kazi wa kawaida, madaktari, maafisa na wakuu wengine wanataka sana kujifunza Biblia.