Ukurasa wa Pili
Mamilioni ya watu wenye moyo mweupe huamini katika miujiza, mizuka, na njozi. Wao humiminika kwenye sehemu zionwazo kuwa takatifu kama hii iliyoonyeshwa hapa katika Fátima, Ureno, wakiwa na tumaini la kupata au kuona ponyo la kimuujiza. Baadhi ya wenye kujitoa sana watatembea kwa magoti yao mpaka wafike mahali hapo patakatifu. Wengi huamini kwamba wameponywa. Lakini watu wengi wenye moyo mweupe huuliza, Je! kweli miujiza na mizuka hii hutoka kwa Mungu? Je! kuna elezo jingine lolote?