Tukio la Kukumbuka!—Jumamosi, Machi 30
Ilikuwa Nisani 14 ya mwaka 33 W.K. Yesu alikuwa akishiriki pamoja na mitume wake kikombe cha divai na mkate usiotiwa chachu. Agizo lake? “Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19, NW. Hivyo basi, mara moja kwa mwaka, Mashahidi wa Yehova kuzunguka ulimwengu wanakusanyika kukumbuka kifo cha Yesu kwa njia aliyoagiza usiku ule alipotoa usemi huo. Mwaka huu, Nisani 14 inaanza Jumamosi, Machi 30, baada ya jua kushuka. Wewe unaalikwa kwa ukunjufu ujiunge na sisi katika mkutano huu wa ukumbuko jioni hiyo ya Jumamosi. Tafadhali pata habari kwa Mashahidi wa Yehova wa kwenu juu ya wakati na mahali penyewe hasa ambapo mkutano utakuwa.