Ukurasa wa Pili
WEWE UMEPATA kutazama picha yako mwenyewe ya wakati ulipokuwa mtoto ukawaza hivi, ‘Kweli maisha ni mafupi sana’? Je! umepata kuuliza hivi kwa mshangao, ‘Je! mimi naweza kuishi muda mrefu kuliko vile ambavyo natarajia sasa?’
Kwa muda mrefu wanadamu wametafuta maisha marefu yenye sulubu ya ujana duniani. Lakini je! tazamio hilo ni fikira ya kuwazia-wazia mazuri tu? Fikiria maoni ya watu fulani ya kutazamia mema, na uchunguze ni kwa nini kuna sababu thabiti za kutazamia mema.