Je! Umepata Kuuliza?
◻ Maoni ya Mungu ni nini juu ya talaka?
◻ Je! Biblia inakubali uasherati au ngono ya watu wa jinsia moja?
◻ Ni kwa nini Mungu ameruhusu taabu?
◻ Je! kweli yeye alikusudia ulimwengu uwe kama ulivyo?
◻ Wakati ujao utakuwa wa namna gani?
Mmoja wa Mashahidi wa Yehova angependezwa kukutembelea na kukusaidia upate majibu ya Biblia kwa maswali hayo. Mashahidi wa Yehova hutoa maagizo ya Biblia kwa mtu binafsi na kwa kikundi bila malipo yoyote.
Kwa hiyo iwapo ungependa mtu anayestahili akutembelee nyumbani mwako au mahali pengine panapokufaa zaidi, sisi tutafurahi kupangia hilo. Utasaidiwa kupata si majibu tu ya maswali yako ya Biblia bali pia ya matatizo ya leo yanayoweza kutatuliwa kwa kutumia kanuni za Biblia. Ili utumikiwe hivyo, jaza tu habari iliyoombwa chini na uipeleke kwa njia ya posta kwenye anwani iliyo chini.