Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?
Viongozi wa jumuiya katika Roma ya karne ya kwanza walimwambia mtume Paulo Mkristo: “Tunataka kusikia kwako uonavyo wewe; kwa maana katika habari za madhehebu hiyo imejulikana kwetu kwamba inanenwa vibaya kila mahali.” (Matendo 28:22) Watu hao walitaka kusikia kutoka chanzo hicho, badala ya kusikia kutoka kwa wachambuzi wa nje peke yao.
Leo, Mashahidi wa Yehova pia hunenewa kinyume, na lingekuwa ni kosa kutazamia kujifunza ukweli juu yao kutoka kwa vyanzo vyenye uonezi. Kwa hiyo twapendezwa kutoa broshua ya kurasa 32 Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya Ishirini, ambayo yaeleza juu ya imani na utendaji mbalimbali wa Mashahidi wa Yehova. Iwapo hiyo ingekupendeza, tafadhali jaza na kupeleka kwa posta kuponi iliyo hapa.
Ningependa habari juu ya broshua yenye kurasa 32 Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya Ishirini.