Sura Ina Maana Gani?
“Nilihangaishwa juu ya sura yangu,” aandika kijana wa kike kutoka Beaver Falls, Pennsylvania, U.S.A “Nilijiona kuwa mwenye uso mbaya na asiye vutia.” Yeye aeleza hivi: “Mimi ningekula kidogo sana kwa siku chache, na nilipoteza ratili kadhaa, lakini nigeona njaa sana kwa ajili ya kutokula hivi kwamba ningejivimbisha kwa chakula siku ifuatayo na kupata uzito tena.”
Baadaye, katika mkusanyiko wa Kikristo, yeye alisema hivi: “Niliangalia ndani ya kioo na kumwambia rafiki, ‘Naonekana vibaya sana!’
“Rafiki huyo mpenzi aliniuliza kama nilikuwa nimesoma sehemu ‘Kuangalia Jinsi Unavyoonekana’ katika kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Nilimwambia hapana. Yeye aliniambia hivi, ‘mpenzi wangu, wewe unahitaji uende nyumbani leo usiku na uisome.’ Nami nilifanya hivyo barabara.
“Niliona kana kwamba ninasoma hadithi ya maisha yangu. Halafu nikafikia swali ambalo lilinifanya nifikirie, ‘Ni nani ambaye hueneza wazo kwamba unahitaji sura fulani ikiwa utakuwa mwenye kupendwa, mwenye kufanikiwa au mwenye furaha?’”
Jibu la swali hilo, kijana huyu alisema, lilifanya mabadiliko yenye kutokeza katika maisha yake. Yeye alimaliza hivi: “Kupitia madokezo yenye kusaidia katika kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, niliona uhitaji wa kupanga vizuri mambo nipaswayo kutanguliza.”
Vijana wana mikazo mingi leo. Wanahitaji msaada ili wakabiliane nayo kwa kufanikiwa. Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi kinaandaa msaada huo. Wewe unaweza kupokea nakala ya kitabu hiki chenye vielezi vya kuvutia kwa kujaza na kupeleka kuponi hii.