Siku ya Kukumbukwa
Jioni iliyotangulia kifo chake, Yesu alishiriki na mitume wake mkate usiotiwa chachu na kikombe cha divai na kusema: “Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19, NW.
Mwaka huu mwadhimisho wa amri yake ni Jumanne, Aprili 6, baada ya jua kutua.
Kama tokeo, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote watakusanyika usiku huo wa pekee ili kurudia Ukumbusho huo kwa njia ile aliyoomba Yesu. Unaalikwa kwa uchangamfu sana uungane nao. Tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova mahali unapoishi ili upate kujua wakati na mahali barabara pa mkutano huo.