Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 5/8 uku. 32
  • “‘Yehova’ Afutwa na Wanazi”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “‘Yehova’ Afutwa na Wanazi”
  • Amkeni!—1993
Amkeni!—1993
g93 5/8 uku. 32

“‘Yehova’ Afutwa na Wanazi”

MANENO hayo yalikuwa ndiyo kichwa kikuu cha gazeti New York Herald Tribune la Novemba 20, 1938. Makala hiyo ilisema hivi: “Makanisa ya Kiprotestanti katika sehemu fulani nchini [Ujerumani] waliamriwa waondoe neno ‘Jehova’—ambalo ni endelezo la Kijerumani la Yehova, linalotokana na ‘Yahweh,’ neno la Kiebrania linalomaanisha Mungu—na pia majina ya manabii wa Kiyahudi katika Agano la kale.”

Hayo yote yalikuwa ni sehemu ya jitihada ya Wanazi ya kunyanyasa Wayahudi. Kwa wakati uo huo, bila shaka ilikusudiwa ipatie Mashahidi wa Yehova pigo, waliokuwa wamepigwa marufuku tangu 1933 na ambao pia walipelekwa katika kambi za mateso.

Katika 1933, kulikuwa na Mashahidi wanaotenda 19,268 katika Ujerumani. Leo, baada ya kuwindwa sana na Wanazi na, kufikia hivi karibuni, na Wakomunisti katika Ujerumani Mashariki, kuna Mashahidi 163,000 wanaoshirikiana na makundi 1,938. Na jina Yehova halijafutwa katika maneno ya Kijerumani. Zeugen Jehovas, Mashahidi wa Yehova, wanajulikana kotekote katika Ujerumani.

Ikiwa ungependa kupata habari zaidi kuhusu Mashahidi, tafadhali tembelea Jumba la Ufalme la mahali penu, au andikia I.B.S.A., Box, 47788, Kenya.

[Picha katika ukurasa wa 32]

Makao makuu ya ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova katika Selters/Taunus, Ujerumani

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki