Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 5/22 uku. 31
  • Maisha Moja ya Pekee

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maisha Moja ya Pekee
  • Amkeni!—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • “Watu Wanasema Kwamba Mimi Ni Nani?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Yesu—Mambo Ambayo Watu Wanasema Kumhusu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Tulifanya Uamuzi Thabiti wa Kuunga Mkono Utawala wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1993
g93 5/22 uku. 31

Maisha Moja ya Pekee

“ALIZALIWA katika kijiji kisichojulikana sana, mtoto wa mwanamke wa maisha ya hali ya chini. Akalelewa katika kijiji kingine tena, ambapo alifanya kazi katika duka la seremala mpaka alipofikia miaka thelathini. Kisha kwa miaka mitatu alikuwa mhubiri wa kuzunguka-zunguka.

“Hakuandika kitabu chochote. Hakuwa na cheo chochote. Hakuwa na familia wala nyumba. Hakwenda chuo. Hakupata kutembelea jiji kubwa. Hakupata kusafiri [kilometa mia tatu na ishirini] kutoka alikozaliwa. Hakufanya yoyote ya yale mambo ambayo watu huhusianisha na ukuu. Hakuwa na barua za ustahili ila yeye mwenyewe.

“Alikuwa na miaka thelathini na tatu tu wakati umma ulimgeuka. Rafiki zake walimtoroka. Alikabidhiwa kwa maadui wake na akapitia hukumu ya dhihaka. Alitundikwa [mtini] katikati ya wezi wawili. Alipokuwa akifa, wauaji wake walipigia kura vazi lake, mali pekee aliyokuwa nayo duniani. Alipokuwa amekufa, alizikwa katika kaburi lililoazimwa kupitia huruma ya rafiki.

“Karne kumi na tisa zimekuja na kupita, na leo anaendelea kuwa mtu mkuu wa jamii ya ainabinadamu, na kiongozi wa maendeleo ya ainabinadamu. Majeshi yote yaliyopata kupiga miguu, na manowari zote zilizopata kuundwa, na mabunge yote yaliyopata kuwa na kikao, wafalme wote waliopata kutawala, wakijumlishwa pamoja hawakupata kuwa na uvutano juu ya maisha za wanadamu katika dunia hii kwa nguvu nyingi kama maisha hiyo moja ya pekee.a”—An anonymous commentary on the life of Jesus Christ.

[Maelezo ya Chini]

a Maelezo zaidi juu ya maisha hiyo ya pekee yanapatikana katika kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, kilichotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki