Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 7/22 uku. 32
  • Mtawa Ajifunza Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mtawa Ajifunza Kweli
  • Amkeni!—1993
Amkeni!—1993
g93 7/22 uku. 32

Mtawa Ajifunza Kweli

Katika Djibouti, Afrika, mtawa Mkatoliki aliyeitwa Louis Pernot alipata kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako kutoka kwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Louis, ambaye alikuwa mwalimu mkuu wa shule moja ya Katoliki, alikuwa amejiuliza mara nyingi kwa sababu gani dini yake haikutoa habari hususa ya kusaidia vijana kukabiliana na matatizo yao.

Jioni hiyo aliyopokea kitabu hicho Louis alianza kukisoma kitabu Ujana Wako. Kwa kweli, alipendezwa nacho sana hivi kwamba hakuweza kuacha kukisoma. Aliwazia kwamba dini ya kweli inapaswa kutoa mwongozo unaofaa kwa watu bila kuridhia mafundisho ya Biblia, na sasa alikuwa amekipata kitabu hicho!

Siku iliyofuata Louis alimwambia Shahidi ambaye alikuwa amempa kitabu hicho kwamba amepata kweli. Wakati wa juma hilohilo, akajiuzulu utawa wake na pia kuwa Mkatoliki. Akawa mmoja wa Mashahidi wa Yehova na kuanza kufundisha kweli za Biblia alizojifunza.

Mashahidi wa Yehova ni tengenezo la ulimwenguni pote la zaidi ya wanafunzi wa Biblia milioni nne ambao wamejitoa kusaidia watu wajifunze zaidi juu ya makusudi ya Mungu. Ikiwa ungependa kupata habari zaidi au kuwa na funzo la Biblia nyumbani bure pamoja na Mashahidi wa Yehova, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki