Faraja kwa Walioshuka Moyo
Mwaka uliopita Mashahidi wa Yehova walitangaza trakti ndogo yenye kurasa sita juu ya habari hiyo inayotajwa juu. Kwa ufupi sana inaandaa aina ya msaada ambao watu walioshuka moyo wanahitaji. Trakti hiyo yaonyesha kwamba Biblia ndiyo chanzo bora zaidi cha faraja. Inataja makumi ya Maandiko yanayofaa juu ya habari ya kushuka moyo, kutia ndani yale yanayoweza kutumiwa kusaidia watu walioshuka moyo.
Mwezi wa Oktoba uliopita ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova katika Rome, Italia, ilipokea simu ambayo mwenye kuipiga alisema hivi: “Nataka kuwashukuru kwa ajili ya trakti inayozungumzia kushuka moyo. Nimeipokea hivi punde, na nikahisi ni lazima niwapigie simu kuwashukuru. Sijapata kusoma kitu chochote chenye kutia moyo hivi katika kichapo chochote cha kitiba. Nataka kuwapongeza kwa sababu mnafaulu kusema mengi sana kwa nafasi kidogo.
“Niliposoma trakti hiyo, nilitokwa machozi. Nataka kuwatia moyo mwendelee na kazi yenu. Ni ya maana; mwapaswa kuifanya kotekote Italia na ulimwenguni pote.”
Ikiwa ungependa kupata nakala ya trakti hiyo, Faraja kwa Walioshuka Moyo, au habari zaidi, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.