‘Sijakutana Kamwe na Mmoja wa Mashahidi wa Yehova Ambaye Sikumpenda’
JE! UMEWAHI kukutana na mmoja wa Mashahidi wa Yehova ana kwa ana? Je! umewahi kupata fursa ya kujua lile wanaloamini kikweli? Labda umewahi kukutana na Shahidi kifupi barabarani au mlangoni mwa nyumba yako. Lakini hilo mara nyingi hukosa kuruhusu wakati wa kuwasiliana vizuri.
George Plagenz, mwandikaji safu za kidini wa U.S., aliandika juu ya yale aliyojionea mwenyewe akiwa na Mashahidi: “Kutumia maneno ya [mcheshi Mwamerika] Will Rogers, ambaye alisema hajakutana kamwe na mtu ambaye hakupenda, sijakutana kamwe na Shahidi wa Yehova ambaye sikumpenda.”
Kisha Plagenz akanukuu mwandishi Mwailandi Alan Bestic: “Washiriki wa tengenezo hilo lenye kusutwa sana ni watu wenye kujumuika, wachangamfu na wenye furaha. Katika kusanyiko lao la kimataifa katika London [Uingereza], nilitendewa kwa fadhili zote, heshima ya uanana na urafiki wa kweli na kila Shahidi niliyekutana naye.”
Plagenz asema kwamba njia za zamani za kwenda mlango kwa mlango za uchokozi za Mashahidi fulani zilitokeza hisia zisizo za kirafiki. “Lakini hayo yote yamebadilika.” Kisha amnukuu msemaji Shahidi: “Wengi walio Mashahidi leo walifunga mlango kwa nguvu usoni pa Shahidi aliyewazuru.” Kwa nini kuna itikio chanya zaidi siku hizi? “Watu wanaanza kutambua . . . kwamba hakuna utatuzi kwa matatizo makubwa ambayo ulimwengu unakabili.”
Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba jibu pekee la matatizo ya ainabinadamu limeonyeshwa katika sala ya Yesu “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Utawala wa Ufalme wa Mungu, unaotambuliwa na familia ya kibinadamu tiifu na yenye upole, ndio utatuzi pekee kwa jeuri na chuki inayofadhaisha ulimwengu sasa. Ikiwa ungependa kujua mengi juu ya Biblia na mafundisho yayo, tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova kwenye Jumba la Ufalme lililoko karibu, au tumia anwani ya karibu zaidi iliyoonyeshwa kwenye ukurasa wa 5.